Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa akikabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa wizara hiyo Mhe. Dkt. Angeline Mabula katika ofisi za Wizara eneo la Mtumba Jijini Dodoma
Mpima Ardhi wa Tume Emmanuel Mwanga akichukua majira nukta kwenye mpaka wa Vijiji vya Gomero na Kichangani, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro wakati wa zoezi la uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji jirani na Hifadhi ya Nyerere
Mtaalamu wa TEHAMA kutoka Tume, Bw. Gerald Mseti (wa pili kulia) akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi namna Mfumo wa Taarifa za Matumizi ya Ardhi (National Land Use Information System – NLUIS) unavyofanya kazi katika utoaji wa Hati za Hakimiliki
Sehemu ya Wananchi wa Kijiji cha Makusi Wilayani Makete wakiwa kwenye Mkutano wa Kijiji kwa ajili ya kujadili na kupitisha mpango wa matumizi ya ardhi wa kijiji hicho
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mh. Antony Mtaka (aliyesimama) akizindua Mkakati wa Kupanga, Kupima Ardhii na kutoa Hati Miliki za Kimila kwa wakulima wa ngano. jumla ya Vijiji 44 vinatarajiwa kuandalimwa mipango ya matumizi ya ardhi na kuandaliwa Hatimiliki
Sehemu ya wananchi wa Kijiji cha Kibuye, Kata ya Bukuba katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe, Mkoani Kigoma wakimsikiliza kwa makini Mtaalamu kutoka Tume wakati wa Mkutano Mkuu kwa ajili ya uandaaji wa Mpango wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji hicho
Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu kutoka Tume mara baada ya utambulisho wa uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji 16 katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime
Watumishi wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) wakiwa kwenye maandamano wakati wa maadhimisho ya sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika Kimkoa katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma
Wapima Ardhi wakiandaa vifaa kwa ajili ya upimaji wa mipaka ya vijiji vilivyohitaji marekebisho ya mipaka, wakati wa zoezi la uandaaji mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji 25 katika Halmashauri za Wilaya ya Itilima, Busega na Meatu Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu Mh. Fauzia H. Ngatumbura akipokea mrejesho kutoka kwa wataalamu wa Tume na Halmashauri mara baada ya kukamilika kwa kazi ya uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji 12 katika Wilaya hiyo.
Mjumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji (aliyesimama) akiwasilisha rasimu ya mpango wa matumizi ya ardhi ya kijiji kwenye mkutano mkuu wa Kijiji cha Sapa
Mpima Ardhi kutoka Tume (Katikati) Bw. Mikidadi Kalimang’asi akiwaongoza wajumbe kutoka vijiji vya Mbushi na Jinamo kwenye kikao cha kujadili mpaka unaowagawanyisha Vijiji hivyo.
Sehemu ya Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Jinamo, Wilayani Meatu, wakiwa kwenye mkutano mkuu wa Kijiji kwa ajili ya kujadili na kupitisha mpango wa matumizi ya ardhi ya kijiji hicho.
Mpima Ardhi wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Bw. Emmanuel Kasitila akiwaongoza wajumbe kutoka vijiji vya Iramba Ndogo na Sungu kupima mpaka baina ya vijiji hivyo.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (wa nne kutoka kushoto) Prof. Wakuru Magigi akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza hilo mara baada ya Kikao cha Baraza kilichofanyika mjini Dodoma.