Mkurugenzi Mkuu Bw. Joseph Constantine Mafuru Wasifu
Mkuu wa Wilaya ya Mlele Alhaj Majid Mwanga akikabidhi Hati ya Hakimiliki ya Kimila kwa mwananchi wa Kijiji cha Mtakuja mara baada ya Kijiji hicho kuwezeshwa kuandaa Mpango wa Matumizi ya Ardhi kupitia Mradi wa Usimamzi Shirikishi wa Miombo -DSL IP 10/1/25
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Mtakuja walionufaika na Hatimiliki wakiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Wilaya ya Mlele, Tume, TFS na Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Katavi mara baada ya kukabidhiwa Hatimiliki hizo na Mkuu wa Wilaya ya Mlele
Ugawaji wa Hati za Hakimiliki za Kimila kwa wananchi wa Kijiji cha Mtakuja zilizoandaliwa kupitia Mradi Shirikishi wa Misitu ya Miombo ya Nyanda Kame Tanzania (Integrated Landscape Management in Dry Miombo Woodlands of Tanzania).
Sehemu ya Wananchi wa Kijiji cha Idetemya kilichopo katika Kata ya Nyabulanda, Wilayani Nyang'hwale wakiwa kwenye Mkutano wa Kijiji cha ajili ya kujadili Mpango wa Matumizi ya Ardhi wa Kijiji hicho uliwasilishwa na Halmashauri ya Kijiji 05/01/2025
Wataalamu kutoka Tume wakiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Geita (Katikati mwenye Tai) mara baada ya mazungumzo juu ya uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 14 Wialayani Nyang'hwale 27/12/2024
Baadhi ya Wananchi wa Vijiji vya Ntilili na Igalukiro Mkoani Katavi wakiwa na nyuso za furaha mara baada ya kupatiwa Hatimiliki zilizoandaliwa na Tume kupitia Mradi wa Urejeshwaji Endelevu wa Mazingira na Uhifadhi wa Bioanuai Tanzania (SLR) 21/11/2024
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akikabidhi Hati ya Hakimili ya Kimila kwa mwananchi wa Kijiji cha Igalukiro katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimwe mara baada ya Kijiji hicho kuandaliwa Mpango wa Matumizi ya Ardhi
Wataalamu wa Tume wakiwa kwenye Kikao Kazi kwa ajili ya maandalizi ya kazi ya Ufuatliaji na Tathmini ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi pamoja na Uzingativu wa uandaji wa Mipango hiyo inayofanyika katika Halmashauri za Wilaya 15 nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru (Katikati - waliosimama) akiwa kwenye picha ya pamoja na ujumbe wa USAID mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo ya namna ya kushirikiana katika kutekeleza sehemu ya Mradi wa USAID TUHIFADHI MALIASILI
Mjumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji akitoa maelezo kwenye Ramani ya Mpango wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji hicho iliyopelekea kuandaliwa kwa Hati za Hakimiliki za Kimila
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Nzega ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Mohamed M. Mtulyakwaku akikabidhi Hati ya Hakimiliki ya Kimila kwa mmoja wa mwananchi wa Kijiji cha Seki katika Halfa ya ugawaji Hatimiliki hizo iliyofanyika katika Kijiji cha Seki
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Seki kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nzega wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni Rasmi mara baada ya kukabidhiwa Hati za Hakimiliki za Kimila 25/10/2024
Baada ya kuandaliwa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji vya Seki na Buduba, wananchi zaidi ya 1,300 wa Vijiji hivyo watapatiwa Hatimiliki za Kimila kwa ajili ya kumiliki ardhi zao Kisheria kuanzia tarehe 25/10/2024
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru (wa pili kushoto) akiwa na Wataalamu wa Tume na Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro alipotembelea kukagua kazi ya uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 14 katika Halmashauri hiyo 22/10/2024
Sehemu ya Wananchi wa Kijiji cha Nambubi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe wakifuatilia uwasilishaji wa Mpango wa Matumizi ya Ardhi wa Kijiji chao 18/10/2024