Albamu ya Video
Utekelezaji wa Mradi wa Upangaji Matumizi ya Ardhi Katika Wilaya ya IGUNGA
Utekelezaji wa Mradi wa Upangaji wa Matumizi ya Ardhi (Land Use Planning Project) pia unatekelezwa katika Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora katika vijiji vinavyopitiwa na Mradi wa Bomba la Mafuta (EACOP) kwa upande wa Tanzania kutoka Mutukura-Kagera hadi Chongoleani-Tanga. Katika Wilaya ya Igunga, jumla ya vijiji 4 (Bulyang’ombe, Igogo, Nyandekwa, Mwabaraturu), Vitovu Vitatu (3) vya Biashara (Ziba, Ibologero na Mwalamo) na maeneo yaliyopo kwenye Mamlaka ya Mji Mdogo wa Igunga (Igunga, Mwanzugi, Makomero na Mgongolo) yenye mitaa 7 inayopitiwa na Mradi wa Bomba la Mafuta. Hadi kufikia tarehe 26 Juni, 2019, mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji 4 vya (Bulyang’ombe, Igogo, Nyandekwa, Mwabaraturu) na Mipango kina ya maeneo ya Ziba, Ibologero, Mwalamo, Kamando, Mwamaganga na Buyumba imeandaliwa na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Igunga.
Imewekwa: Jun 28, 2019
Participatory mapping in the village land use process in Tanzania
Short documentary on the use and benefits of low-tech geospatial method in participatory mapping in village land use process in Tanzania. Hear how the method is being used by district planners to facilitate participatory mapping with village representatives, and how both planners and villagers see the approach as increasing participation and planning quality
Imewekwa: Jun 28, 2019
Uzinduzi wa Mradi wa Upangaji wa Matumizi ya Ardhi Kitaifa Katika Kijiji cha Sojo, Wilayani Nzega
Mradi wa Upangaji wa Matumizi ya Ardhi (Land Use Planning Project) ni mradi unaohusu upangaji wa matumizi ya ardhi katika Wilaya na vijiji vinavyopitiwa na Mradi wa Bomba la Mafuta (EACOP) kwa upande wa Tanzania kutoka Mutukura-Kagera hadi Chongoleani-Tanga; Wilaya na Vijiji ambavyo vinapakana na Nchi jirani kote nchini; na Wilaya na vijiji vilivyokuwa na kambi za wakimbizi katika Mikoa ya Tabora na Katavi. Mradi huu unatekelezwa na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika kipindi cha Miaka Mitatu kuanzia mwaka wa fedha 2018/19 hadi 2021/22. Jumla ya Wilaya 38 na vijiji 1502 vinatarajiwa kuandaliwa mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji katika kipindi husika. Awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huu imeanza mwezi Aprili 2019 katika wilaya 13 ukihusisha vijiji vyote vinavyopitiwa na Mradi wa Bomba la Mafuta kwa upande wa Tanzania. Wilaya hizo ni Misenyi, Bukoba, Muleba, Chato, Bukombe, Mbogwe, Igunga, Iramba, Singida, Chemba, Kiteto, Handeni na Muheza. Jumla ya vijiji 226 vinatarajiwa kuandaliwa mipango ya matumizi ya ardhi ambapo maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama vile kilimo, malisho ya mifugo, makazi ya watu, hifadhi za vyanzo vya maji na misitu, uwekezaji pamoja na huduma za jamii yanatarajiwa kutengwa.
Imewekwa: Jun 16, 2019
Utekelezaji wa Mradi wa Upangaji wa Matumizi ya Ardhi katika Wilaya ya Kiteto
Mradi wa Upangaji wa Matumizi ya Ardhi (Land Use Planning Project) ni mradi unaohusu upangaji wa matumizi ya ardhi katika Wilaya na vijiji vinavyopitiwa na Mradi wa Bomba la Mafuta (EACOP) kwa upande wa Tanzania kutoka Mutukura-Kagera hadi Chongoleani-Tanga; Wilaya na Vijiji ambavyo vinapakana na Nchi jirani kote nchini; na Wilaya na vijiji vilivyokuwa na kambi za wakimbizi katika Mikoa ya Tabora na Katavi. Mradi huu unatekelezwa na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika kipindi cha Miaka Mitatu kuanzia mwaka wa fedha 2018/19 hadi 2021/22. Awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huu imeanza mwezi Aprili 2019 katika wilaya 13 ukihusisha vijiji vyote vinavyopitiwa na Mradi wa Bomba la Mafuta. Katika Wilaya ya Kiteto, jumla ya vijiji 14 vinatarajiwa kuandaliwa mipango ya matumizi ya ardhi ambapo maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama vile kilimo, malisho ya mifugo, makazi ya watu, hifadhi za vyanzo vya maji na misitu, uwekezaji pamoja na huduma za jamii yanatarajiwa kutengwa.
Imewekwa: Jun 13, 2019
Rais Magufuli ahimiza upangaji na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amehimiza upangaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi kama nyenzo muhimu katika kutatua migogoro ya ardhi nchini na kuwapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kwa kufanya juhudi za kupanga matumizi ya ardhi katika vijiji vyao.
Imewekwa: Sep 12, 2018
Tume kuandaa kanzidata ya taarifa za matumizi ya ardhi
Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi imeanza kuandaa kanzidata ya taarifa za matumizi ya ardhi nchini. Kanzidata hii itatunza na kutoa taarifa za wadau wanaojihusisha na upangaji, utelelezaji wa matumizi ya ardhi katika maeneo mbalimbali nchini pamoja na taarifa za mipango ya matumizi ya ardhi iliyoandaliwa na wadau mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wake
Imewekwa: Sep 08, 2018