Mkurugenzi Mkuu Bw. Joseph Constantine Mafuru Wasifu
Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale, Mhe. Grace Kingalame, akikabidhi tuzo kwa Mkurugenzi wa Upangaji Matumizi ya Ardhi, Usimamizi na Uratibu (DLUPMC), Bw. Jonas Masingija, kutambua mchango wa Tume katika kuwezesha uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi
Mtaalamu kutoka Tume, Bi. Esther Rapemo, akitoa elimu kuhusu Sheria za Rasilimali Ardhi kwa wananchi wa Kijiji cha Pashungu, Wilayani Mbeya, wakati wa zoezi la utambulisho wa uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 8, lililofanyika 16/01/2026
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Timetheo Mzava akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Wizara ya Ardhi kilichokuwa na lengo la kuifahamu Wizara ya Ardhi na Taasisi zake kilichofanyika 15/01/2026.
Waziri wa Ardhi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, ameongoza kikao cha Menejimenti ya Wizara hiyo ambapo walijadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ardhi na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kazi pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi mara baada ya kuizindua katika hafla iliyofanyika Dodoma 17/12/2025
Waziri wa Ardhi, Numba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo akimkabidhi vitendea kazi mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika tukio la uzinduzi wa Kamati hiyo lililofanyika Jijini Dodoma 17/12/2025
Sehemu ya Wataalamu wa Mipango Miji na Vijiji kutoka Tume walioshirki Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wataalamu wa Mipango Miji uliofanyika Jijini Mwanza Novemba 27&28, 2025
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru akimuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Antony Sanga kufunga Mkutano wa 10 wa mwaka wa Wataalamu wa Mipango Miji na Vijiji uliofanyika Jijini Mwanza tarehe 27&28/11/2025
Mkurugenzi wa Utafiti, Uzingatiaji na Mifumo Dkt. Joseph Paul, akifanya wasilisho kuhusu upangaji wa matumizi ya ardhi wakati wa kikao na ujumbe kutoka International Cooperation and Consultancy Center (ICCC) kilichofanyika tarehe 26 Novemba 2025.
Prof. Rocky Wen kutoka Taasisi ya International Cooperation and Consultancy Center (ICCC) ya China akitoa uzoefu kuhusu Upangaji wa Matumizi ya Ardhi nchini humo, wakati wa kikao cha pamoja kati ya ICCC na Tume kilichofanyika Jijini Dodoma, 26/11/2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Leonard Douglas Akwilpo (MB) kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dodoma 18/11/2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Kaspar Kaspar Mmuya (MB) kuwa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dodoma 18/11/2025
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru akiwasilisha Mada kuhusu Upangaji Matumizi ya Ardhi katika moja ya Mijadala inayoendelea kwenye Mkutano wa 30 wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP30) Belem, Brazil 13/11/2025
Kuhakikisha Haki za Umiliki wa Ardhi kwa Uhimilivu wa Tabianchi Tanzania: Suluhisho za Kidijitali kwa Umiliki Jumuishi, Uhimilivu wa Ikolojia na Ukuaji Endelevu wa Miji. #COP30
Mkurugenzi Mkuu wa Tume akiwa na Washiriki wengine katika Mkutano wa 30 wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP30) unaofanyika Belem, Brazil kuanzia Novemba 10 hadi 21, 2025.