Mkurugenzi Mkuu Bw. Joseph Constantine Mafuru Wasifu
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mradi wa Upangaji Matumizi ya Ardhi mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, walipofanya ziara ya kukagua Mradi huo katika Kijiji cha Ubembe, Muheza,
Afisa Ardhi Mkuu wa Tume Adv. Otmary Komba akitoa elimu juu ya Upangaji, Usimamizi na Utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa wananchi wa Kijiji cha Taigo, Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mkoani Manyara 13/03/2026
Wanawake kutoka Tume wakipata mbele ya Mgeni Rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary S. Senyamule wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mbande, Wilayani Kongwa 08/03/2026.
Wanawake kutoka Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi wakiwa tayari kwa ajili ya kusherehekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambapo Kimkoa yalifanyika katika Wilaya ya Kongwa tarehe 08/03/2026
Naibu Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa Kaspar Mmuya, akikabidhi hati ya umiliki kwa mwananchi wa Kijiji cha Namagondo wakati wa hafla ya ugawaji wa hatimiliki hizo iliyofanyika kijijini hapo tarehe 16 Februari 2026.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume, Bw. Joseph Mafuru, akitoa taarifa ya kazi ya uandaaji wa Hati za Hakimiliki za Kimila (CCROs) kwa wananchi wa vijiji viwili Wilayani Ukerewe mbele ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, 16/2/26
Mkurugenzi Mkuu wa Tume akisaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) mbele ya Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa Programu ya FORLAND, yenye lengo la kuwezesha uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji zaidi ya 160 katika Mikoa minne nchini.
Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale, Mhe. Grace Kingalame, akikabidhi tuzo kwa Mkurugenzi wa Upangaji Matumizi ya Ardhi, Usimamizi na Uratibu (DLUPMC), Bw. Jonas Masingija, kutambua mchango wa Tume katika kuwezesha uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi
Mtaalamu kutoka Tume, Bi. Esther Rapemo, akitoa elimu kuhusu Sheria za Rasilimali Ardhi kwa wananchi wa Kijiji cha Pashungu, Wilayani Mbeya, wakati wa zoezi la utambulisho wa uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 8, lililofanyika 16/01/2026
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Timetheo Mzava akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Wizara ya Ardhi kilichokuwa na lengo la kuifahamu Wizara ya Ardhi na Taasisi zake kilichofanyika 15/01/2026.
Waziri wa Ardhi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, ameongoza kikao cha Menejimenti ya Wizara hiyo ambapo walijadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya ardhi na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kazi pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi mara baada ya kuizindua katika hafla iliyofanyika Dodoma 17/12/2025
Waziri wa Ardhi, Numba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo akimkabidhi vitendea kazi mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika tukio la uzinduzi wa Kamati hiyo lililofanyika Jijini Dodoma 17/12/2025
Sehemu ya Wataalamu wa Mipango Miji na Vijiji kutoka Tume walioshirki Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wataalamu wa Mipango Miji uliofanyika Jijini Mwanza Novemba 27&28, 2025
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru akimuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Antony Sanga kufunga Mkutano wa 10 wa mwaka wa Wataalamu wa Mipango Miji na Vijiji uliofanyika Jijini Mwanza tarehe 27&28/11/2025