Mkurugenzi Mkuu Bw. Joseph Constantine Mafuru Wasifu
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru, akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji (VLUM) wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa zoezi la uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji Wilayani Morogoro.
Afisa Ardhi Mkuu wa Tume Robin Wambura, akitoa mafunzo kuhusu Upangaji na Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi kwa wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Muungano, Wilayani Morogoro, ikiwa ni sehemu ya zoezi la uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji
Wataalamu kutoka Tume wakiwajengea uwezo wajumbe wa Timu ya Upangaji Shirikishi wa Matumizi ya Ardhi (PLUM) ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kabla ya kuanza zoezi la uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji katika Halmashauri hiyo
Ujumbe wa Tume ukiwa katika picha ya pamoja na wakufunzi wa Chuo Kikuu cha Twente, Kitivo cha ITC, kufuatia ziara ya mafunzo na kubadilishana uzoefu uliolenga kuimarisha uwezo katika upangaji na usimamizi wa matumizi ya ardhi.
Wataalamu kutoka Tume wakipata mafunzo ya vitendo kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa katika upangaji wa matumizi ya ardhi, ikiwemo matumizi ya mifumo ya taarifa za kijiografia (GIS) wakati wa ziara ya Chuo cha Twente nchini Uholanzi
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo (Mb) akisisitiza jambo kwa Wadau wakati akifungua Jukwaa la Wadau wa Matumizi ya Ardhi (Land Use Mult-stakeholder Forum) Mjini Morogoro, tarehe 12/05/2026
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru (katikati) akiongoza Kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume kilichofanyika tarehe 07/05/2026
Watumishi wa Tume wakiwa kwenye shamrashamra za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani (Meimosi) yaliyofanyika Kimkoa katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma 01/05/2026
Mkurugenzi Mkuu wa Tume, Bw. Joseph Mafuru, akiongoza kikao kati ya NLUPC na IUCN kujadili utekelezaji wa mradi wa Nature-Based Solutions pamoja na kubainisha fursa mpya za ushirikiano katika masuala ya mipango ya matumizi ya ardhi na uhifadhi wa mazingir
Wahadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Twente nchini Uholanzi wakipata maelezo kutoka kwa viongozi wa Kijiji cha Selela Wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha, wakati wa ziara ya mafunzo kuhusu utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi katika nyanda za malisho.
Wahadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Twente nchini Uholanzi wakiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi na Watumishi wa Tume mara baada ya kumaliza kikao kazi kuhusu matumizi ya GIS na fursa za ushirikiano kati ya Tume na Chuo hicho, kilichofanyika Jijini Dodoma
Wakufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Twente nchini Uholanzi wakitoa mada kuhusu matumizi ya GIS na fursa za ushirikiano kati ya Tume na Chuo hicho, wakati wa kikao kazi na wataalamu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi kilichofanyika Jijini Dodoma.
Sehemu ya wananchi wa Kijiji cha Majojoro, Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, wakishiriki mkutano wa kijiji kwa ajili ya mchakato wa uandaaji wa Hati za Hakimiliki za Kimila (CCROs) kupitia uwezeshaji wa Tume kwa kushirikiana na shirika la ADAP.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume Bw. Joseph Mafuru akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mradi wa Upangaji Matumizi ya Ardhi mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, walipofanya ziara ya kukagua Mradi huo katika Kijiji cha Ubembe, Muheza,
Afisa Ardhi Mkuu wa Tume Adv. Otmary Komba akitoa elimu juu ya Upangaji, Usimamizi na Utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa wananchi wa Kijiji cha Taigo, Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mkoani Manyara 13/03/2026